FEISAL SALUM ABDALLAH (Fey Toto) NI MCHEZAJI MWENYE KIPAJI CHA MPIRA WA KUZALIWA..
- Simon Kimanga
- 2024-03-23
FEISAL SALUM ABDALLAH (Fey Toto) NI MCHEZAJI MWENYE KIPAJI CHA MPIRA WA KUZALIWA..
- Simon Kimanga
- 2024-03-23
kijana mbakaji maarufu anaswa mkoani Iringa. |
Huko mkoani
Iringa kumeibuka tukio lililosababisha taharuki kubwa miongoni mwa wakazi wa
Kitasengwa na Ilala ambapo watoto wadogo wa kike na kiume kuripotiwa kubakwa na
kulawitiwa kwa kipindi kifupi.
Na katika
matukio yote hayo imebainika kumuhusisha kijana mmoja tu aliyejulikana kwa jina
moja tu la “Blasistus” Haikuwa kazi
rahisi kumnasa kijana huyu kwa jinsi alivyo nadhifu na mtanashati mbele ya
jamii ya wengi katika maeneo hayo anayo ishi, hupendelea sana kuvaa kofia aina
ya “kapero” na kibegi cha rangi nyeusi.
Yeye ni
mwajiliwa wa shirika la usambazaji wa madawa nchini Tazania MSD. Na ni
mwanakwaya ya Mshindo ya Kanisa Katoliki, na watu wa karibu naye wamedai kuwa
yeye ni moja kati ya vijana wanao ishi na virusi vya Ukimwi. Arobaini yake
ilifika siku alipomlawiti mtoto wa kiume wa miaka 14 wa baba mwenye nyumba wake,
baada ya kumuadhibu kwa bakora za kutosha baba wa mtoto huyo aliamua kumpeleka
katika kituo cha polisi ambapo bado ameshikiliwa akisubili hatua zaidi za
kisheria. Na Simon Kimanga Mkoani Iringa. |